Visit Website

Kwa mahitaji ya mitihani, Maazimio ya kazi, Shajara, Notes, na materials mbalimbali ya kielimu, wasiliana nasi ujipatie huduma zetu kwa gharama nafuu sana.

Tunatoa huduma za materials mbalimbali za kielimu kwa gharama nafuu wasiliana nasi leo..

[PDF] nukuu za somo kiswahili darasa la tatu

PFF download nukuu za somo kiswahili darasa la tatu | Nukuu za somo kiswahili pdf download | nukuu za somo pdf download | nukuu za somo shule ya msing

Sura ya 01 : Sauti zinazounda maneno

Ukijifunza sura hii utaweza kusoma silabi na maneno yenye sauti za herufi gh, py, nz, sw, lw, ky, tw, ng’w, nyw nashw.

Huu ni mwendelezo wa sauti za herufi ulizojifunza darasa la pili.

Kusoma na kuandika maneno yenye sauti za herufi

gh, lw, py, nz, sw na tw.

Soma kwa sauti maneno haya.

(a) ghali (b) Kulwa (c) nzi (d) swali (e) twanga

(f) mpya (g) gharama (h) Kilwa (i) nzige (j) swala

(k) tweta (l) jipya (m) ghairi (n) Nzega (o) swaga (p) kutwa

(a) ghali (b) Kulwa (c) nzi (d) swali (e) twanga

(f) mpya (g) gharama (h) Kilwa (i) nzige (j) swala

(k) tweta (l) jipya (m) ghairi (n) Nzega (o) swaga (p) kutwa

Soma habari hii, kisha jibu maswali yanayofuata.

Darasa jipya

Neema na Kulwa ni marafiki. Wote wanasoma katika Shule ya Msingi Mkwajuni. Mwaka jana walikuwa darasa la pili. Mwaka huu wameingia darasa la tatu. Shule ya Msingi Mkwajuni ilifunguliwa wiki ya kwanza ya mwezi Januari. Siku ya kufungua shule wanafunzi wote walifika shuleni mapema. Walifanya usafi wa mazingira ya shule, kisha wakasimama mstarini.

Swaiba alikuwa mwalimu wa zamu. Aliwasalimia wanafunzi na kuwatakia heri ya mwaka mpya. Aliwaeleza kuwa kila mwanafunzi anapaswa kusoma kwa bidii. Aidha, anapaswa kuzingatia sheria za shule. Aliwaeleza wanafunzi kuwa vyumba vya madarasa vimebadilika. Wanafunzi waliokuwa darasa la kwanza mwaka uliopita, wataingia chumba cha darasa la pili.

Wanafunzi waliokuwa darasa la pili wataingia chumba cha darasa la tatu. Baada ya matangazo, wanafunzi waliingia madarasani.

Wanafunzi wa darasa la tatu walianza mwaka wakiwa na furaha. Kila mwanafunzi alikuwa na hamu ya kuanza kusoma katika darasa jipya. Walipoingia darasani, mwalimu wa darasa aliwaongoza kuchagua viongozi. Neema alichaguliwa kuwa dada wa darasa na Ghalibu kuwa kaka wa darasa.


Maswali

1. Rafiki yake Neema anaitwa nani?

2. Neema na rafiki yake wanasoma shule gani?

3. Nani alikuwa mwatimu wa zamu?

4. Kwa nini wanafunzi wa darasa la tatu watikuwa na furaha?

Zoezi la 1

1. Soma kwa sauti maneno yaliyokolezwa wino katika habari uliyosoma.

2. Unganisha sauti za herufi gh tw py nz sw tw na a e i o u kuunda silabi.

Mfano Ukiunganisha sauti ya herufi gh na sauti ya herufi a unaunda silabi gha

(a) gh a gha

(b) lw - -

(c) nz --

(d) sw --

(e) tw - -

3. Tenganisha silabi zilizounda maneno.

Mfano

  • wanafunzi wa na fu nzi
  • waliaswa wa li a swa
  1. walianza
  2. jipya
  3. anapaswa

4. Tenganisha sauti za herufi katika sitabi.

Mfano : pya - py a

  1. swa
  2. nzu
  3. ghi
  4. lwa
  5. twe

1. Soma maneno yafuatayo kwa sauti.

(a) ghala (b) ghorofa (c) funza (d) kwanza (e) panzi (f) rut (g) kanzu (h) kitanzi
(i) nzige (j) swati (k) sweta (l) swata (m) mswaki (n) jipya (o) mpya (p) upya (r) Kilwa (s) Kulwa (t) twanga (u) tweta (v) twiga (w) twisha (y) patwa (z) kutwa

Zoezi la 3

Soma sentensi zifuatazo kwa sauti.

(a) Mwalimu amewauliza wanafunzi maswali.

(b) Baba amenunua nguo kwa bei ghali.

(c) Mwanafunzi ameanza kwenda shuteni.

(d) Huu ni mwaka mpya.

(e) Mjomba amejenga nyumba ya ghorofa.

(f) Kilwa ni mji mzuri.

(g) Kaka yake Kulwa anaitwa Mpetwa.

Zoezi la 4

Tunga sentenst mbiti kwa kila neno.

(a) mpya (b) ghati (c) swati (d) nzuri (e) Kutwa

Soma mazungumzo kati ya Sungura na Chui, kisha fanya mazoezi.


Sungura Habari za leo kaka Chui.

Chui Nzuri!

Sungura Leo umekunywa maji?

Chui Sijanywa maji.

Sungura Ooh! itabidi nimuagize Pweza atuletee maji kutoka baharini, "Leo bahari ni shwari".

Chui Hapana! Kuna binadamu anayeitwa Ng'wale anauza maji.

Sungura Inaonekana humpendi Pweza.

Chui Si kweli! Sina uadui na Pweza.

Sungura Nafikiri tuwaache wote. Tuagize maji kutoka kwa Kyando.

Chui Nakubaliana na wewe. Maji anayouza Kyando ni safi sana.

Sungura Kweli! Itabidi tununue hayo.

Chui Sawa mdogo wangu.

Zoezi la 5

Andika maneno yenye sauti za herufi zifuatazo kutokana na mazungumzo utiyoyasoma.

(a) ky (b) pw (c) ng'w (d) nyw (e) shw (f) nz

Zoezi la 6

1. Tafuta maneno yenye sauti za herufi nyw shw pw nz tofauti na mazungumzo utiyosoma.

Mfano

  • nyw - nywele
  1. shw -
  2. pw -
  3. nz -

2. Soma kwa sauti silabi hizi.

(a) pwa (b) kya (c) ng'wa (d) pwi (e) nywa (f) shwi (g) kye (h) shwa (i) ng'wi (j) Kyo (k) ng'we (() nywe

3. Soma kwa sauti sentensi hizi.

(a) Bibi yangu anaishi Kyela.

(b) Baba anapenda kula pweza.

(c) Mzee Ng'wandu amejenga nyumba nzuri.

(d) Hali ya bahari ni shwari.

Zoezi la 7

Andika maana za maneno yafuatayo kwa kuchagua jibu sahihi.

Mfano shwari — hali ya ututivu.

Maneno Maana
  1. shwari
  2. ghali
  3. pweza
  4. kitanzi
  5. uadui

(i) kamba au uzi utiofungwa kwa duara

(ii) yenye bet kubwa

(iii) halt ya kutendeana ubaya baina ya watu

(iv) kiumbe wa baharini

(v) hali ya ututivu


Sura Ya 2 : Matamshi Ya Herufi

Katika sura hii utajifunza kutamka, kusoma na kuandika maneno yenye sauti za herufi s na th, z na dh, t na r, g na gh kwa usahihi.

Kutamka maneno yenye sauti za herufi s na th kwa usahihi.

Tazama picha na namba zifuatazo, kisha fanya zoezi tinatofuata.

Zoezi la 1

1. Tamka majina ya vita unavyoviona katika picha namba 1 hadi 5.

2. Tamka kwa sauti namba 80 na 30

3. Taja sauti ya mwanzo inayosikika unapotamka maneno samaki, sabuni, sarafu na saa.

4. Taja sauti ya mwanzo inayosikika unapotamka namba 80 na 30.

Zoezi la 2

Soma maneno yafuatayo kwa sauti.

(a) saa (b) sahani (c) subiri (d) soko (e) safari (f) sabuni (g) saruji (h) msumari (i) usafi (j) pasi (k) fenesi (t) msusi (n) thetathini (n) themanini (o) thamani (p) thubutu (r) theluji (s) urithi

Zoezi la 3

Nakili sentensi zifuatazo katika daftari tako. Kisha chagua neno sahihi kwa kupigia mstari.

  • Mfano (Samaki, thamaki) ni chakula bora.

(a) Mimi ninaoga kwa kutumia maji safi na (sabuni, thabuni)

(b) Tuna anaishi karibu na (thoko, soko).

(c) Mwanafunzi mtiifu amepata alama (semanini, themanini).

(d) Mimi ninapenda kuta (fenesi, fenethi).

(e) Bibi huosha (sahani, thahani) kabla ya kuweka chakula.

Kutamka maneno yenye sauti za herufi z na dh kwa usahihi

Tazama picha zifuatazo kisha fanya zoezi

Zoezi la 4

1. Tamka majina ya vitu unavyoviona katika picha namba 1 na 2.

2. Taja sauti ya mwanzo inayosikika unapotamka maneno haya.

(a) zawadi zutia zahanati zeze zao zabibu

(b) dharau dhaifu dhoofu dhoruba

Zoezi la 5

Soma kwa sauti maneno haya.

(a) ziwa (b) mnazi (c) zeze (d) zizi (e) zuia (f) nazi (g) zito (h) zamani (i) mzazi (j) maziwa (k) dhoofu (l) dharura (m) madhara (n) dhahabu (o) adhabu (p) dhambi (r) dhuru (s) dhuluma (t) dhoruba (u) dharau

Zoezi la 6

Kamilisha sentensi zifuatazo kwa kuchagua neno sahihi.

Mfano Dhahabu hupatikana Tanzania. (zahabu, dhahabu)

1. Mimi ninapenda kupiga . . . . . . . . (dheze, zeze)

2. Gunia litilojaa viazi ni . . . . . . . . . . (dhito, zito)

3. Pamba ni . . . . . . . . . la biashara. (zao, dhao)

4. Mama alisema kuwa kuiba ni . . . . . . . . (dhambi, zambi)

5. Tuma alikwenda kuwatembelea . . . . . . . . wake. (wadhazi, wazazi)

Kutamka maneno yenye sauti za herufi l na r kwa usahihi.

Soma kwa sauti maneno haya.

(a) ladha (b) lazima (c) Linda (d) lain (e) lami (f) elea (g) lima (h) mali (i) Liza (j) alika (k) kalia (L) koroboi (m) barabara (n) ridhia (o) redio (p) rika (r) jeraha (s) raba (t) robo (u) rudi (v) bure (w) roho (y) ruhusa (z) riadha

Zoezi la 8

Tazama picha zifuatazo, kisha tunga sentensi mbili kwa kilo picha.

Mfano

1. Huu ni mlango.

2. Nyumba yetu ina mlango mzuri.

Zoezi la 9

I. Andika maneno yafuatayo kwa usahihi.

Mfano zuli — zuri

(a) bule . . . . . . . (b) ria . . . . . . .

(c) rami . . . . . . . . (d) ledio . . . . . . . . . .

(e) luhusa . . . . . . . . .

(f) balabala . . . . . . . . . .

(g) loho . . . . . . . . . (h) jelaha . . . . . . . . .

2. Soma kwa sauti maneno uliyoandika katika swali la kwanza.

Kutamka maneno yenye sauti za herufi g na gh kwa usahihi.

Soma kwa sauti maneno haya

(a) gari (b) gauni (c) ugali (d) fagio (e) gego (f) gitaa (g) goti (h) gunia (i) guta (j) ugua (k) ghali (I) ghala (m) lugha (n) ghorofa (o) gharama

Zoezi la 11

Taza nafasi zilizoachwa wazi kwa kutumia herufi g au gh. Kisha soma kwa sauti maneno haya.

(a) —ari (b) — ali

(c) lu — a (d) —unia

(e) —ogo (f) —arama

(g) u — ua (h) —ala

(i) —asia (j) — oti

(k) — itaa (t) — orofa

1. Nakili jedwali la maneno yafuatayo katika daftari lako. Kisha weka alma ya vema ( ✔ ) kwa kila neno sahihi na kosa ( ✖ ) kwa neno lisilo sahihi.

samaki gorofa dhambi ruka
zawadi subiri thoko ziwa
saruji sabuni gali sukari
dhiwa ledio lugha dhulumu
thamaki ulithi rara luhusa

2. Orodhesha maneno yote yasiyo sahihi kutoka katika jedwali la swali la kwanza. Yaandike maneno hayo kwa usahihi.

Mfano ledio — redio

Post a Comment

Visit Website
Visit Website